Vyombo vya habari vyatakiwa kuepuka habari za kuchonganisha
Vyombo vya habari vimetakiwa kuwa makini na kuepuka kuandika habari
zinazohusu imani za kidini kwa kuegemea upande mmoja ama kwa majumuisho
ili kuepusha kuchochea chuki miongoni mwa jamii.
“ Jambo hilo ni muhimu siyo tu kwa manufaa ya taaluma bali pia kwa kulinda amani na umoja katika Taifa’, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam leo.
Mukajanga, alisema kuwa kumeibuka uandishi usiozingatia uhalisia, ulinganishi na umahususi badala yake uandisi unachukua mfumo wa kuegemea upande mmoja na kufanya majumuisho yasiyotokana na ukweli uliothibitishwa na mwandishi.
“Mapungufu hayo ya kiweledi”, alisema, “yamesababisha habari nyingi kuwa potofu na chonganishi”.
Alisema kuwa weledi hautaki kwa mfano gazeti kumhoji sheikh mmoja au kadhaa au askofu mmoja au kadhaa na kuandika vichwa vya habari vinavyosema “ Waislamu wataka….” au “ Wakristo wakata..”.
“Ikiwa yanayosemwa ni mawazo ya kiongozi mmoja wa dini ni bora isemwe hivyo. Dhehebu linaweza kuhusishwa tu ikiwa yeye ni msemaji rasmi na anaongea kwa niaba ya dhehebu hilo”, alisema Mukajanga.
Vichwa vya habari kama “Maaskofu wamng’oa Naibu Meya Arusha” huku kukiwa `hakuna ushahidi wowote ndani ya habari yenyewe unaoashiria kuwa kujiuzulu kwa huyo Naibu Meya kulitokana na shinikizo la maaskofu ni upotoshaji unaoweza kusababisha chuki, amesema Mukajanga.
Mbaya zaidi, Mukajanga alisema, ni pale kesho yake gazeti jingine linapowatafuta masheikh na kuwaomba kauli yao kuhusiana na kung’olewa kwa Naibu Meya kulikofanywa na maaskofu.
“Ni wazi hapa kuna hatari ya ya wanahabari kugeuka wachonganishi”, alisema Mukajanga.
Pia alisema kumewahi kuchapishwa kichwa kilichosema “ Masheikh wawaonya maaskofu”. Hii ni hatari, alisema.
Mukajanga pia alisema habari nyingine ilidai bila uthibitisho wowote kuwa waumini wa Kanisa Katoliki wametengwa na Kanisa hilo kwa kujihusisha na chama fulani cha siasa. Viongozi wa kanisa hilo hawakuhojiwa, alisema.
Hivi karibuni, Mukajanga alisema, gazeti moja liliandika “Waislamu: Osama hajafa – wadai kuzikwa haraka ni dalili za kuficha ukweli”.
Mukajanga alihoji hivi ni kweli maoni kwamba Osama hajafa yalikuwa maoni ya waislamu wote nchini?
Pia aliuliza baada ya Al-Qaeda wenyewe kukiri kuwa Osama kafa, gazeti hilo halikusikia vibaya kwamba limewasababishia dhihaka Waislamu wote bila uhalali wowote lilipowasingizia kwamba wamesema Osama hajafa?
Gazeti lingine, Mukajanga alisema lilimnukuu mchungaji mmoja aliyepinga ukaguzi wa mahesabu ya makanisa na kuandika kichwa cha habari kilichosema “Makanisa yakataa kukagulkiwa na serikali”.
Hata hivyo Mukajanga alisema, baadaye katibu wa makanisa hayo yaliyotajwa alinukuliwa akisisitiza kuwa yale yalikuwa mawazo binafsi ya mchungaji huyo.
Mukajanga alinukuu kifungu cha 1.9 cha kanuni za maadili kwa wahariri (uk5) kuzuia ubaguzi kinachosisitiza: Hakikisha habari hazilengi wala kutoa nafasi kwa ubaguzi wa kijinsia, dini makundi ya watu wachache, umri, kabila…”
Kuhusu dini , alisema, kifungu 1.14 (uk6) kinaelekeza: Zungumza na mashrikia ya dini, yape haki sawa na heshima yanayostahili kwani hadhi za wawakilishi, viongozi, waumini na imani zao zinapaswa kuheshimiwa na kuthaminiwa.
mwisho
“ Jambo hilo ni muhimu siyo tu kwa manufaa ya taaluma bali pia kwa kulinda amani na umoja katika Taifa’, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam leo.
Mukajanga, alisema kuwa kumeibuka uandishi usiozingatia uhalisia, ulinganishi na umahususi badala yake uandisi unachukua mfumo wa kuegemea upande mmoja na kufanya majumuisho yasiyotokana na ukweli uliothibitishwa na mwandishi.
“Mapungufu hayo ya kiweledi”, alisema, “yamesababisha habari nyingi kuwa potofu na chonganishi”.
Alisema kuwa weledi hautaki kwa mfano gazeti kumhoji sheikh mmoja au kadhaa au askofu mmoja au kadhaa na kuandika vichwa vya habari vinavyosema “ Waislamu wataka….” au “ Wakristo wakata..”.
“Ikiwa yanayosemwa ni mawazo ya kiongozi mmoja wa dini ni bora isemwe hivyo. Dhehebu linaweza kuhusishwa tu ikiwa yeye ni msemaji rasmi na anaongea kwa niaba ya dhehebu hilo”, alisema Mukajanga.
Vichwa vya habari kama “Maaskofu wamng’oa Naibu Meya Arusha” huku kukiwa `hakuna ushahidi wowote ndani ya habari yenyewe unaoashiria kuwa kujiuzulu kwa huyo Naibu Meya kulitokana na shinikizo la maaskofu ni upotoshaji unaoweza kusababisha chuki, amesema Mukajanga.
Mbaya zaidi, Mukajanga alisema, ni pale kesho yake gazeti jingine linapowatafuta masheikh na kuwaomba kauli yao kuhusiana na kung’olewa kwa Naibu Meya kulikofanywa na maaskofu.
“Ni wazi hapa kuna hatari ya ya wanahabari kugeuka wachonganishi”, alisema Mukajanga.
Pia alisema kumewahi kuchapishwa kichwa kilichosema “ Masheikh wawaonya maaskofu”. Hii ni hatari, alisema.
Mukajanga pia alisema habari nyingine ilidai bila uthibitisho wowote kuwa waumini wa Kanisa Katoliki wametengwa na Kanisa hilo kwa kujihusisha na chama fulani cha siasa. Viongozi wa kanisa hilo hawakuhojiwa, alisema.
Hivi karibuni, Mukajanga alisema, gazeti moja liliandika “Waislamu: Osama hajafa – wadai kuzikwa haraka ni dalili za kuficha ukweli”.
Mukajanga alihoji hivi ni kweli maoni kwamba Osama hajafa yalikuwa maoni ya waislamu wote nchini?
Pia aliuliza baada ya Al-Qaeda wenyewe kukiri kuwa Osama kafa, gazeti hilo halikusikia vibaya kwamba limewasababishia dhihaka Waislamu wote bila uhalali wowote lilipowasingizia kwamba wamesema Osama hajafa?
Gazeti lingine, Mukajanga alisema lilimnukuu mchungaji mmoja aliyepinga ukaguzi wa mahesabu ya makanisa na kuandika kichwa cha habari kilichosema “Makanisa yakataa kukagulkiwa na serikali”.
Hata hivyo Mukajanga alisema, baadaye katibu wa makanisa hayo yaliyotajwa alinukuliwa akisisitiza kuwa yale yalikuwa mawazo binafsi ya mchungaji huyo.
Mukajanga alinukuu kifungu cha 1.9 cha kanuni za maadili kwa wahariri (uk5) kuzuia ubaguzi kinachosisitiza: Hakikisha habari hazilengi wala kutoa nafasi kwa ubaguzi wa kijinsia, dini makundi ya watu wachache, umri, kabila…”
Kuhusu dini , alisema, kifungu 1.14 (uk6) kinaelekeza: Zungumza na mashrikia ya dini, yape haki sawa na heshima yanayostahili kwani hadhi za wawakilishi, viongozi, waumini na imani zao zinapaswa kuheshimiwa na kuthaminiwa.
mwisho
No comments:
Post a Comment