*DK.
SLAA AZUIWA KUOA*-Rose Kamili Anayedai Kuwa Ni Mke Wa Katibu Mkuu Wa
CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa, Amefungua Kesi Mahakama Kuu Akiiomba
Isimamishe Ndoa Ya Kiongozi Huyo Na Mke Mwingine Inayotarajiwa Kufungwa
Julai 21 Mwaka Huu Wilayani Karatu, Mkoa Wa Manyara. Dk Slaa Anatarajia
Kufunga Ndoa Na Mchumba Wake Wa Siku Nyingi, Josephine Mushumbusi. Rose
Kamili Mbunge Wa Chadema Pia Anaiomba Mahakama Iamuru Dk. Slaa Amlipe
Shs Mil. 50 Za Fidia Aliyotumia Kujihudumia Pasipo Matunzo Ya Mumewe
Huyo. Mbunge Huyo Kupitia Kwa Wakili Wake Joseph Thadayo, Anaiomba Pia
Mahakama Iamuru Josephine Mushumbusi Amlipe Kiasi Cha Shs Mil. 500 Za
Fidia Ya Maumivu Aliyoyapata Kutokana Na Kitendo Chake Cha Kuingilia
Ndoa Yao. Kesi Hiyo Namba 4 Ya Mwaka 2012 Iliyopangwa Kusikilizwa Na
Jaji Lawrance Kaduli Inatarajia Kutajwa
Kwa Mara Ya Kwanza Leo. Katika Hati Hiyo Ya Madai, Mbunge Huyo Anadai
Kuwa Ndoa Inayotarajiwa Kufungwa Kati Ya Dk. Slaa Na Josephine
Mushumbusi Ni Batili Kwa Sababu Kuna Ndoa Nyingine Halali Na
Inayoendelea Kuishi Kati Ya Slaa Na Rose Iliyofungwa Mwaka 1985. Alidai
Baada Ya Kufungwa Kwa Ndoa Hiyo Juni 18, 1987 Walifanikiwa Kupata Mtoto
Wa Kike Anayeitwa Emiliana Slaa Na Badaye Septemba 23, 1988 Walipata
Mtoto Mwingine Wa Kiume Aitwaye Linus Slaa. Katika Uhusiano Wao Dk. Slaa
Akiwa Padri Wa Kanisa Katoliki Alifanya Taratibu Za Kujiondoa Katika
Nafasi Hiyo Na Kuanza Maisha Ya Familia. TAFAKARI..