Saturday, June 16, 2012

JESHI LA POLISI KANDA MAALUMU TARIME RORYA LAKAMATA WATU 74 WANAODAIWA KUVAMIA MGODI WA DHAHABU NYAMONGO ABG.


14-Jun-12                                  

 Watu  74 wanaotuhumiwa kwa  kuvamia  mgodi wa ABG North Mara wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga na mishale kwa nia ya kuiba mawe ya dhababu wamekamatwa na Jeshi la polisi   Kanda Maalum ya TARIME/RORYA.

 Kamanda wa polisi kanda maalumu ya TARIME RORYA ACP JUSTUS KAMUGISHA amesema kitendo hicho cha wananchi kuvamia mgodi ni kosa la jinai na watuhumiwa wote waliokamatwa watafikishwa mahakamani ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mgodi wa ABG North Mara bado unaandamwa na uvamizi wa watu wakiwa na silaha za jadi kwa kile kinachodaiwa kutaka kuiba mawe yanayosemekana kuwa na dhahabu.


Akiongea na waandishi wa Habari Mkuu wa Oparesheni wa Jeshi la Polisi Nchini Kamishna Msaidizi Mwandamizi SIMON SIRRO amesema jeshi hilo pamoja na kukamata wavamizi, pia limefanya mazungumzo na viongozi pamoja na wazazi ili kutafuta suruhu ya kudumu itakayo komesha tatizo la uvamizi wa Mgodi,  tatizo ambalo amekili kuwa ni la muda mrefu na wazazi wasiposhirikishwa katika kutafuta njia muafaka ya kumaliza mgogoro huu uliopo kati ya wananchi wanaoishi kuzunguka eneo la mgodi wa ABG North Mara ''Nyamongo'' basi tutegemee hadithi ilele iliyodumu zaidi ya muongo mmoja sasa.








No comments:

Post a Comment